0
Ziara ya Kilimanjaro Music Tour ambayo ndio gumzo kubwa sasa katika sekta ya

burudani imebisha hodi katika Mji wa Moshi ambapo wapenzi wa muziki wanatarajiwa

kupata burudani ya aina yake kutoka kwa wasanii mbalimbali Jumamosi hii.

 Maandalizi yote yamekamilika huku zaidi ya wasanii 10 wa humu nchini wakitarajiwa

kutua mjini hapo Ijumaa tayari kwa show kubwa itakayofanyika katika Viwanja vya Chuo

Shirikishi cha Ushirika na Biashara (MUCCOBs).

Ziara hii inadhaminiwa na Bia ya Kilimanajro Premium Lager ambayo imekuwa mstari

wa mbele katika kufikisha muziki wa Tanzania kwenye kilele cha mafanikio. Ziara hii

inaratibiwa na EATV na East Africa Radio, Executive Solutions, Integrated na AIM.

Wasanii watakaotoa burudani ni pamoja na Ommy Dimpoz, Kala Jeremiah, Weusi, Ben

Pol, Jambo Squad, Young Killer, Ney wa Mitego, Mwana FA, Khadija Kopa, Warriors na

Professor J.

“Wasanii wote wako tayari kutoa burudani ya aina yake na sisi kama wadhamini

tunawaahidi wakazi wa Moshi mambo mazuri...waje kwa wingi wakutane na wasanii

wao na pia wapate burudani bila kusahau Bia yao namba moja Kilimanjaro Premium

Lager,” alisema Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, George Kavishe.

Alisema kiingilio katika show hii itakayoanza saa nne asubuhi ni Tsh 2500 na kila

atakayeingia atapewa bia ya bure mradi ametimiza umri wa miaka 18 na show itaanza

saa nne asubuhi hadi saa kumi na mbili jioni.

Tiketi wa ajili ya show hii zitaanza kuuzwa siku ya Ijumaa pale MUCCOBs na pia

promosheni mbalimbali za kusisimua zinaendelea katika baa tofauti Mjini Moshi.

“Ziara hii sio ya washindi wa Tuzo za Muziki (Kilimanjaro Music Awards) bali ni ziara ya

wasanii ili waweze kutangaza kazi zao pamoja na kupeleka burudani mikoani ili watu

wanaokaa huko pia waweze kufaidi,” alisema Bw Kavishe.

Aliongeza kuwa wasanii wana nafasi kubwa sana kueneza ujumbe mbalimbali katika

jamii hivyo wanapaswa kuungwa mkono ili waweze kuwafikia wananchi wakiwemo wa

mikoani.

Ziara hii itahusisha mikoa ya Moshi, Mwanza, Kigoma, Kahama, Iringa, Mbeya,

Dodoma, Tanga, Mtwara na Dar es Salaam na inaanzia Mkoani Moshi Mei 24, Mwanza

Mei 31, Kahama Juni 7, Kigoma Juni 14, Iringa Juni 21, Mbeya Agosti 9, Dodoma

Agosti 16, Tanga Agosti 23, Mtwara Agosti 30, Dar es Salaam Septemba 6,” alisema

Kavishe.
ASANTE KWAKUTEMBELEA WEBSITE  HII JIUNGE NASI  KUWA MWANA FAMILIA WA JIMMCARTER.COM FACEBOOK-JIMCARTERTZ | TWITTER JIMMCARTERTZ

Post a Comment

 
Top