RIP: Watanzania wamlilia Edwin Semzaba, mwandishi wa kitabu cha Ngoswe
Mwandishi wa vitabu vya Kiswahili kikiwemo, Ngoswe: Penzi Kitovu cha Uzembe, Edwin Semzaba amefariki dunia Jumapili ya January, 17.
Alikuwa mhadhiri wa chuo kikuu cha Dar es Salaam, UDSM kwenye idara ya sanaa za maonesho. Semzaba anakumbukwa kwa uandishi wake mahiri hususan kwa kitabu cha mchezo wa Ngoswe; Penzi Kitovu cha Uzembe kilichotumika kwenye shule za sekondari katika somo la Kiswahili.
Marehemu Edwin Semzaba, kulia
Baadhi ya vitabu vya hadithi alivyoandika ni pamoja na Marimba ya Majaliwa, 2008, Funke Bugebuge, 1999, Tausi wa Alfajiri, 1996 na Tamaa ya Boimandaa, 2002
Michezo aliyoiandika ni pamoja na Kinyamkera, 2014, Joseph na Josephine, , 2014, Mkokoteni, 2014, Tendehogo na Sofia wa Gongolambotoa 1985.
Semzaba amewahi kushinda tuzo nyingi za uandishi wa vitabu.
Hivi ndivyo watu walivyotuma salamu zao za rambirambi.
Tumepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa za kifo cha mwanafasihi mahiri ndg. Edwin Semzaba tunawapa pole Watanzania wote pic.twitter.com/716Cepoonn
— Taifa Kwanza ✋ (@ACTwazalendo) January 18, 2016
Mungu Amlaze Pema Mwandishi Huyu Edwin Semzaba.
#NgoswePenziKitovuChaUzembe
— Mecky Kaloka (@NgomeVideo) January 17, 2016
Kapumzike kwa amani Mzee Edwin Semzaba 🙏🏽 pic.twitter.com/LFzBiRj7A1
— Lameck Ditto (@Lameckditto) January 17, 2016
TANZIA: Edwin Semzaba, Mwandishi wa kitabu maarufu cha Ngoswe - Penzi Kitovu cha Uzembe amefariki dunia leo... pic.twitter.com/NwKFxZvUfA
— Jamii Forums (@JamiiForums) January 17, 2016
Nimesikitishwa sana na kifo cha Ndugu, mtu wangu wa karibu Mzee Edwin Semzaba. Sitaki kuamini lakini Mungu amekupenda zaidi. #RIPEdSemzaba
— Mrisho Mpoto (@MrishoMpoto) January 17, 2016
Post a Comment