0
Wizkid tayari anaishi ile ndoto ambayo wasanii wengi wa Afrika bado wanaiota. Kutoka kushirikishwa kwenye wimbo wa Drake ‘One Dance’ uliopo kwenye album Views na ulioshika namba moja kwenye chart za Billboard 100, hadi sasa kuongezwa kwenye orodha ya wasanii watakaomsindikiza Chris Brown kwenye ziara yake ya ‘One Hell of A Nite Tour’ barani Ulaya.

Taarifa hiyo ilitolewa na Chris Brown mwenyewe kwenye akaunti yake ya Instagram kabla ya Wizkid naye kuandika: 5th – 11th June I’ll be supporting my brother @chrisbrownofficial !! Get ur tickets!! #Onehellofanitetour Bringing the African wave!!”

Wizkid ana wimbo aliomshirikisha muimbaji huyo wa Marekani mwenye mashabiki wengi.

Post a Comment

 
Top